Lema ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo amesema mara kadhaa Mbowe amekuwa na nia ya kupumzika na kuwaachia nafasi vijana lakini wanachama wamekuwa wakimshauri    kuendelea kuwa katika nafasi hiyo.

Amesema anamuheshimu sana Mbowe kwa kazi kubwa aliyoifanya hasa ya kukijenga chama hicho lakini anamuomba kwa sasa asikilize ushauri wa familia yake inayomtaka kutogombea nafasi hiyo.