Subscribe Us

Breaking News

Mchezaji Ibra Bacca Sasa ni Sajenti, Apandishwa Cheo na Jeshi Zanzibar


Mchezaji Ibra Bacca Sasa ni Sajenti, Apandishwa Cheo na Jeshi Zanzibar



Mchezaji wa Yanga SC, Ibrahim Hamad #IbraBacca, amepewa heshima kubwa baada ya Kikosi Maalumu cha Kuzuia Magendo (KMKM) #Zanzibar kumpandisha cheo kutoka Koplo hadi Sajenti.

Taarifa hii imetangazwa rasmi na klabu ya #Yanga, wakimpongeza Bacca kwa juhudi na mchango wake uwanjani. Kupandishwa cheo kunathibitisha sio tu uwezo wake katika soka, bali pia nidhamu na bidii alizoonyesha kama mwanajeshi wa KMKM.

Mashabiki wa Yanga na wapenzi wa soka wameendelea kumpongeza kwa mafanikio haya, wakiamini kuwa hatua hii itampa motisha zaidi kuendelea kung’aa ndani ya kikosi cha Wananchi.


Download/Pakua/Install App ya Abedijr kupitia google crome Bofya Hapa

                               app hii aipatikani google playstore ka sasa hupatikana kwenye wavuti yetu hii 

No comments