Subscribe Us

Breaking News

Baraza Kuu la AU lamuidhinisha Faure Gnassingbé wa Togo kuwa mpatanishi kati ya Rwanda na DRC


h

CHANZO CHA PICHA,AFP

Maelezo ya picha,Faure Gnassingbé lazima kwanza aidhinishwe na Baraza Kuu la Wakuu wa Nchi na Serikali la Umoja wa Afrika.

Rais wa Angola João Lourenço jana aliwasilisha mrithi wake kuwa mpatanishi wa mzozo kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Rwanda.

Rais wa Angola João Lourenço Jimamosi aliwasilisha jina la Faure Gnassingbé, rais wa Togo, kwa kama mridhi wake katika upatanishi wa Rwanda na DRC katika mzozo wa DRC, lengo likiwa ni kumaliza vita katika eneo la masharik mwa DRC.

Alikuwepo katika mkutano wake wa kwanza wa Umoja wa Afrika kama Mkuu wa Nchi wa Umoja wa Afrika, uliofanyika jana, Jumamosi, tarehe 5 Aprili , 2025, kwa kutumia kwa njia ya mawasiliano ya video.

Rais Lourenço alitangaza kwamba mazungumzo ya awali kati yake na Rais Gnassingbé yalileta matokeo chanya, akimaanisha kwamba Togo inakubali kile ilichoombwa.

Wakati wa mkutano huu, Rais Lourenço kwanza alirejelea sababu ya kujiuzulu kwake kama mpatanishi, akisema kwamba alitaka kujitolea kwa majukumu yake kama mkuu wa Umoja wa Afrika.



Download/Pakua/Install App ya Abedijr kupitia google crome Bofya Hapa

                               app hii aipatikani google playstore ka sasa hupatikana kwenye wavuti yetu hii 

No comments