apate muda wa kucheza. Yote yanaweza kutokea hayo.”
Kwa hivyo kwa tafsiri nyepesi ni kwamba ripoti ya Chyna itaamua ‘yuko fiti kiasi gani’, na Pedro ataamua ‘anafaa kiasi gani’ na hivyo hao wawili wataamua abaki ama aondoke Yanga sc.
Kwanini Yao Amezua Mjadala Mkubwa?
Kabla ya kuingia kwenye majeraha, Yao alishawahi kutazamwa kama beki wa kulia mwenye uwezo mkubwa, nguvu, kasi na uwezo wa kupandisha mashambulizi. Alikuwa moja ya “project players” wa Yanga waliokua wanatarajiwa kufanya makubwa zaidi.
Mara kadhaa, benchi la ufundi liliwahi kuhimiza kuwa Yao anaweza kuwa msaada kwa muda mrefu akicheza sambamba na mastaa kama Aucho,Dickson Job na Pacome Zouzoua. Hata hivyo, majeraha ndiyo yaliyokatisha safari yake na kumtoa kwenye hesabu za msimu huu.
Kwa sasa, kutokana na presha ya mechi za Ligi Kuu na CAF Champions League, Yanga wanatafuta depth ya kutosha kwenye nafasi hiyo. Yao akirudi kwenye ubora wake, anaweza kuiongezea timu ushindani na upana wa kikosi.
Changamoto Kubwa Nani Ataondoka Ili Yao Aingie?
Hii ndiyo pointi ngumu kwa sababu nafasi mojawapo lazima itoke kwa mchezaji wa kigeni ili kukidhi matakwa ya wachezaji 12 wa kigeni hasa katika ligi kuu japo kimataifa kanuni bado inaruhusu zaidi ya wachezaji 12.
Kwa ratiba ya misimu iliyopita, mara nyingi Yanga wamekuwa wakifanya maamuzi mazito ya kuachana na mchezaji wa nje ambaye hajatimiza matarajio. Lakini safari hii, karibu wageni wote wa kikosi wanaonekana kutumika mara kwa mara na kuaminiwa na benchi la ufundi.Hivyo, uamuzi wa kuachana na mmoja wao si mwepesi na unaweza kuibua mjadala mpya zaidi.
Mambo Matatu Yatakayoamua Hatima ya Yao
1. Hali ya kiafya na utimamu wake
Chyna Mokaila ndiye mtu muhimu hapa. Atatoa ripoti kuhusu uwezo na uthabiti wa misuli, hatari ya kurejea kwenye majeraha na muda anaoweza kutumika uwanjani bila hatari.
2. Mahitaji ya kiufundi ya Pedro
Pedro anataka nini kwenye mfumo wake? Je, anahitaji beki wa kulia anayepanda na kushuka kwa kasi au anahitaji mtu wa nidhamu ya ulinzi kwanza? Kama Yao hana sifa anazoangalia, nafasi yake itakuwa finyu.
3. Kasi ya kurejea kwenye ubora wa kitambo
Yanga wanapambana kwenye mashindano mbalimbali. Hawana muda wa kusubiri miezi mingine miwili au mitatu kumsubiri mchezaji kuwa “full sharp”. Wanaweza tu kumrudisha kama yuko tayari kucheza mara moja.
Yote Yafunguka Dirisha Dogo Likifunguliwa
Hali ya Yao itajulikana ndani ya wiki chache zijazo. Kwa sasa, mashabiki wanasubiri kwa hamu kuona kama kijana huyo wa Ivory Coast atarejea rasmi kambini kama sehemu ya masplan ya Yanga au kama atachukuliwa kama “project” ya muda mrefu ya kupewa muda wa mkopo ili apate muda wa kucheza ikizingatiwa sasa Israel Mwenda anafanya vizuri kwenye nafasi hiyo.
Download/Pakua/Install App ya Abedijr kupitia google crome Bofya Hapa
app hii aipatikani google playstore kwa sasa hupatikana kwenye wavuti yetu hii

0 Comments:
Post a Comment