Umeme Wakatika Muhimbili Kwa Saa 15, Wagonjwa Wahaha

Umeme wakatika Muhimbili kwa saa 15, wagonjwa wahaha
Dar es Salaam. Wagonjwa wanaopokea huduma ya kuchuja damu ‘dialysis’ katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, MNH wamelalamikia jengo la watoto hospitalini hapo kukosa umeme kwa saa 15 mfululizo, hali iliyoathiri matibabu yao.
Matibabu ya dialysis kawaida hujumuisha kutumia mashine kuchukua kazi ya figo kuchuja sumu, taka na maji kupita kiasi kutoka mwilini. Tiba hii huhitajika kwa wagonjwa ambao figo zao hazifanyi kazi vizuri au zilizofeli.
Akijibu suala hilo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano MNH, Aminiel Aligaesha amekiri kutokea kwa hitilafu hiyo na kueleza hatua zinazochukuliwa kwa sasa.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Mwananchi leo Jumatatu, Mei 26, 2025 wagonjwa hao wamesema umeme huo ulikatika jana saa tatu usiku, kabla ya kuwashwa jenereta ambalo nalo liliharibika baada ya muda mfupi.
Wagonjwa hao ambao hawakutaka kutajwa majina yao kwa sababu za kiusalama, wamesema hali hiyo imesababisha baadhi yao kuanza kupata athari hasi kwa kuvimba miguu, matumbo na kutapika.
“Jengo lote umeme ulikatika jana usiku saa tatu, jenereta likawashwa nalo likazima, wanasema ni mbovu, wameleta mafundi wanatengeneza lakini watu wa Tanesco (Shirika la Umeme Tanzania) hawajafika mpaka sasa hatuna matibabu, hata wagonjwa waliokuwa ICU wamehamishiwa kwenye majengo mengine,” amesema mmoja wa wagonjwa hao.
Amesema hakuna matibabu yanayoendelea kwa sasa, “Wagonjwa wa figo tuko nje tumekaa tu, viongozi wanapita wanatuambia kama unajisikia hauko vibaya sana unaweza kwenda kupumzika nyumbani.”
Mgonjwa mwingine amesema eneo lote la jengo watoto hakuna huduma inayoendelea kwa sasa na yeye amefika toka jana hajafanikiwa kupata huduma.
“Watu wamezidiwa, wengine wapo hoi kabisa na hatujui chochote kinachoendelea, ratiba yangu ilibidi niwe nimepata matibabu mzunguko wa saa 4 usiku, lakini mpaka sasa nimenasa hapa sijapata matibabu.
“Kiukweli kadri masaa yanavyosogea wagonjwa wanaanza kuchoka, sisi figo zote zimekufa tunategemea hizi mashine, wengine wameshazidiwa matumbo yamejaa, miguu imevimba, wengine wanatapika, watoto huko juu wako hoi wamehamishwa wodi wengine wamepelekwa wodi zingine,” amesema.
Mkazi wa Tegeta ambaye hakutaka kutaja jina lake, amesema mtoto wake amelazwa katika moja ya wodi na wamepambana na giza usiku kutokana na kukosekana


No comments