Subscribe Us

Breaking News

Maandamano Tanzania: Wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama wote wawajibike, yasema TEC




Acv

Chanzo cha picha,TEC

Maelezo ya picha,Rais wa baraza la maaskofu Tanzania Wolfgang Pisa

Baraza la maaskofu wa Kanisa katoliki nchini Tanzania limetaka mamlaka zinazohusika ziendelee kulaani mauaji yaliyofanyika na kukiri waliouawa ni watanzania.

Rais wa baraza la maaskofu, Wolfgang Pisa akisoma tamko hilo kuhusu maandamano yaliyoshuhudiwa hivi karibuni, amesema Kuuawa kwa watu hovyo, ukosefu wa demokrasia ni miongoni mwa sababu za watu kuandamana.

“Wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama wote wawajibike, au kuwajibishwa na mamlaka zao za uteuzi. Hasira ya Wananchi ipo katika kuona hakuna anayewajibika kwa matendo maovu waliyofanyiwa raia”. Askofu Wolfgang Pisa, Rais wa TEC.

Amesema kwakuwa jambo hilo limesababisha maafa, baraza linashauri ufanyike uchunguzi utakaowashirikisha wadau wa ndani na nje ya nchi likipendeza wadau kutoka tume huru isiyofungamana na upande wowote kama jumuiya na taasisi za kimataifa,dini na asasi za kiraia na wataalamu wa haki na mambo ya kidemokrasia na serikali iwe tayari kupokea na kufanyia kazi ripoti watakayotoa.

Hapo jana akizungumza na BBC John Heche makamo mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani CHADEMA alisema “Tunahitaji tume huru,kutoka Umoja wa mataifa au Umoja wa Afrika au SADC lakini kwanza tunataka kujua idadi ya watu waliouawa, majeruhi na baadhi ambao hawajulikani walipo’’.

Akihutubia bunge, Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan alitangaza kuwa serikali imeunda tume maalumu kuchunguza matukio yaliyotokea wakati wa maandamano hayo.

"Serikali imechukua hatua ya kuunda tume itakayochunguza kwa undani kilichotokea ili tujue kiini cha tatizo. Taarifa ya tume hiyo itatuongoza katika mazungumzo ya kuleta maridhiano na kudumisha amani," alisema.

Aidha alitangaza msamaha kwa vijana waliokamatwa kufuatia maandamano ya siku tatu yaliyofanyika kuanzia siku ya uchaguzi, Oktoba 29, 2025.

 

Download/Pakua/Install App ya Abedijr kupitia google crome Bofya Hapa

                               app hii aipatikani google playstore kwa sasa hupatikana kwenye wavuti yetu hii 

No comments