Subscribe Us

Breaking News

Mashirika ya kutetea haki za binadamu yaitaka ICC kuichunguza serikali ya Tanzania


Rais Samia

Chanzo cha picha,Getty Images

Muungano wa kimataifa wa wanasheria na makundi ya haki za binadamu umeiomba rasmi Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kumchunguza rais wa Tanzania, na serikali yake kwa uhalifu dhidi ya ubinadamu unaodaiwa kufanywa wakati wa uchaguzi Mkuu wa hivi karibuni.

Waraka wa Ombi kwa ICC linamtuhumu Rais Samia Suhulu Hassan na maafisa wengine wa ngazi za juu kwa kuhusishwa moja kwa moja na vifo vya raia wakati wa maandamano ya baada ya uchaguzi.

Juma lililopita Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan alizindua tume ya uchunguzi kuhusu vurugu hizo baada ya kuwatuhumu wapinzani na mashirika yasiyo ya kiserikali kwa kusababisha machafuko.

Ombi la kuchunguza ukatili unaodaiwa kufanywa na serikali ya Tanzania liliwasilishwa rasmi kwa ofisi ya mwendesha mashtaka wa ICC mnamo Novemba 13 lakini limetangazwa hadharani leo tu.

Hati hiyo yenye kurasa 82 pia inaelezea kile ilichokiita ukiukwaji wa kimfumo na unaoendelea, katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita ikiwa ni pamoja na utekaji nyara, mateso kwa watu waliopotezwa na mauaji ya wapinzani kinyume cha sheria.

ICC bado haijathibitisha kama itafanya uchunguzi. Tanzania ni mwanachama wa chombo hicho.

Rais Samia alishinda zaidi ya asilimia 97 ya kura katika uchaguzi uliowazuia wagombea wakuu wa upinzani kugombea. Maandamano ya baada ya uchaguzi yalisababisha kufungwa kwa intaneti, amri ya kutotoka nje na vifo na kukamatwa kwa mamia ya watu. Makundi ya waangalizi wa kikanda na kimataifa yalielezea uchaguzi huo kama usio wa kidemokrasia.

No comments