Gallery

2/08/2026

 Mfalme wa Zulu Afrika Kusini, amezua gumzo baada ya kutoa matamshi ya kuwadhalilisha raia wa kigeni, na kuwataka waondoke nchini humo.

Mfalme huyo alitoa semi hizo wakati ambapo alitarajiwa kutoa hotuba itakayowatuliza watu wanaowapinga raia wa kigeni katika wilaya yake ya KwaZulu-Natal.

Onyo: Taarifa hii ina mmaelezo ambayo yanaweza kukukera

Misuzulu kaZwelithini alikuwa akiwahutubia wafuasi wake katika eneo ambalo wapiganaji 20,000 wakizulu waliwashinda wanajeshi 1,800 wa Uingereza miaka 147 iliyopita, chini ya mlima wa Isandlwana .

Vita vya Isandlwana, ambavyo vilitokea wakati jamii ya Wazulu ilikuwa inawapinga Waingereza, ni jambo ambalo Wazulu hujivunia pakubwa; kuwa walipigana dhidi ya jeshi la Uingereza na kushinda vita hivyo.

Hasira ya mfalme Misuzulu na watu wake, ameilekeza kwa wahamiaji kutoka mataifa jirani kama Lesotho, Msumbiji na Zimbabwe ambao wameingia Afrika Kusini kutafuta nafasi za ajira.

Kulingana na takwimu, taifa hilo ni nyumbani kwa takriban wahamiaji million 2.4, ambao ni 4% ya idadi ya watu nchini humo.

Mfalme huyo mwenye umri wa miaka 51, hakuchochea vita ila alisema "kwerekwere",neno la kuwadunisha wahamiaji na

0 Comments:

Post a Comment