Ahmed Arajiga Aula Kuchezesha Mechi Kombe la Dunia
WAAMUZI wa Tanzania Ahmed Arajiga, Kassim Mpanga, Said Hamdani na Salum Nasir wameteuliwa na na Shirikisho la soka Duniani (FIFA) kuchezesha mchezo wa Kundi G wa kuwania kufuzu Kombe la Dunia 2026 kati ya wenyeji Botswana dhidi ya Algeria utakaopigwa Mjini Francistown Nchini Botswana Machi 21, 2025.
Algeria na Msumbiji wapo kileleni mwa Kundi G wakiwa na pointi 9 kila mmoja wakifuatiwa na Botswana, Guinea, na Uganda wenye pointi 6 kila mmoja huku Somalia ikiburuza mkia bila pointi yoyote

.jpg)

No comments