
Mamlaka ya China imetangaza hatua za kulipiza kisasi dhidi ya maagizo ya Trump ya kutoza ushuru zaidi kwa bidhaa zinazoingizwa nchini humo.
Hatua za kulipiza kisasi zitajumuisha ushuru wa asilimia 15 kwa makaa ya mawe na gesi asilia kutoka Marekani.
Mafuta ghafi, mashine za kilimo, malori na magari ya injini kubwa zitatozwa ushuru wa asilimia 10.
Tangazo hili limetolewa muda mfupi baada ya ushuru mpya wa asilimia 10 wa Donald Trump dhidi ya China kuanza kutumika.
Wakati huo huo, Idara ya Utawala ya Soko ya China imesema inachunguza kampuni ya Google kwa madai ya kukiuka sheria zake za kupambana na ushindani.
Kampuni hiyo, ambayo haina mashiko vizuri China, ina shughuli ndogo nchini humo.
Beijing ilikosoa ushuru huo katika taarifa Jumapili na kuapa "kutetea kwa uthabiti haki zake" kwa kuwasilisha malalamiko kwa Shirika la Biashara Ulimwenguni (WTO) na kuchukua "hatua zinazolingana."
Aidha, wizara ya biashara ya China imethibitisha kwamba imewasilisha hatua za ushuru zinazotekelezwa na utawala wa Trump kwa utaratibu wa utatuzi wa migogoro wa WTO.
"Hatua za Marekani zinadhoofisha sana mfumo wa biashara wa pande nyingi unaozingatia sheria, inadhoofisha msingi wa ushirikiano wa kiuchumi na kibiashara kati ya China na Marekani, na kuvuruga uthabiti wa viwanda na usambazaji wa kimataifa," wizara hiyo ilisema.
0 Comments:
Post a Comment