Subscribe Us

Breaking News

Liverpool kumuuza Diaz ili kupata mshambuliaji – Tetesi za soka Jumamosi


,

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Liverpool watamuuza Luis Diaz ili kupata fedha za kumnunua mshambuliaji, Manchester City kuwaondoa uwanjani wachezaji na Arsenal yaanzisha tena azma ya kumnunua Dusan Vlahovic.

Liverpool watamuuza mshambuliaji wa Colombia Luis Diaz, 28, msimu huu ili kufadhili usajili wa mshambuliaji. (Football Insider)

.

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Manchester City itawaondoa uwanjani wachezaji ambao hawawezi kuendelea na ratiba yao kwa sababu ya majeraha au uchovu, pamoja na walio katika tishio wakiwemo kiungo wa kati wa Ubelgiji Kevin de Bruyne, 33, na mlinzi wa Uingereza John Stones, 30. (Guardian).

Arsenal wanamtafuta tena mshambuliaji wa Juventus Dusan Vlahovic, 25, huku klabu yake ya Italia ikiwa tayari kumuuza Mserbia huyo kwa kitita cha euro 40m (£33m). (CaughtOffside).

.

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Manchester United, Liverpool na Chelsea wote wanafuatilia uhamisho wa Real Madrid msimu wa joto yenye kumwinda mlinzi wa RB Leipzig na beki wa Ufaransa Castello Lukeba, ambaye kitita chake cha kuweza kumchukua ni milioni 90 (Daily Briefing by Christian Falk - subscription required)

West Ham wamefufua nia yao ya kumnunua mshambuliaji wa Lille na Canada Jonathan David, 25, ambaye anapatikana kwa uhamisho wa bure msimu huu wa joto. (Guardian)

No comments