Msemaji wa jeshi na mwanajeshi wauawa katika shambulio la ndege isiyo na rubani ikulu

Msemaji wa jeshi ameuawa katika shambulio la ndege isiyo na rubani ya RSF kwenye ikulu ya rais, jeshi linasema.
Luteni Kanali Hassan Ibrahim ameuawa pamoja na Kapteni Emad Eldein Hassan, mfanyakazi mwenzake mwenye cheo cha chini , jeshi limeiambia BBC. Kapteni Hassan alikuwa mmoja wa washawishi maarufu wa mitandao ya kijamii wa jeshi.
Wafanyakazi watatu wa kituo cha televisheni cha Sudan pia waliuawa walipokuwa wakiripoti kuhusu harakati za wanajeshi hao kuelekea ikulu. Walikuwa mhariri wa vipindi, mpiga picha na dereva.
Mashambulizi hayo ya ndege zisizo na rubani yalilenga wanajeshi waliokuwa wakisherehekea ndani ya Ikulu ya Republican, saa chache baada ya wanajeshi kuliteka tena jengo hilo la mfano kutoka kwa RSF.

Download/Pakua/Install App ya Abedijr kupitia google crome Bofya Hapa
app hii aipatikani google playstore ka sasa hupatikana kwenye wavuti yetu hii



No comments