'Sherehe ya goli haikulenga kumkejeli Ronaldo' - Hojlund

Rasmus Hojlund alitetea shangwe yake baada ya kutoka kwenye benchi na kufunga bao la ushindi kwa Denmark dhidi ya Ureno akisema hakuwa akimdhihaki Cristiano Ronaldo.
Fowadi huyo wa Manchester United alifunga kwa utulivu baada ya kuunganisha krosi ya Andreas Skov Olsen na kupata ushindi huo katika mkondo wa kwanza wa robo fainali ya Ligi ya Mataifa.
Alisherehekea bao hilo kwa kuiga jinsi Ronaldo anavyosherehekea mabao yake.
"Haikuwa kumdhihaki yeye au kitu chochote, nimekuwa nikisema amekuwa na umuhimu mkubwa kwangu na maisha yangu ya soka," Hojlund alikiambia kituo cha utangazaji cha Denmark TV2.
"Ninacheza dhidi ya mwanasoka bora zaidi duniani na kufunga na kuwa mshindi wa [mechi], haiwezi kuwa bora zaidi.
"Kufunga dhidi yake na Ureno ni kitu kubwa, nilienda kumuona 2009, ambapo alifunga kwa mkwaju wa fauli, na nimekuwa shabiki wake tangu wakati huo."
Nyota wa zamani wa Manchester United na Real Madrid Ronaldo, ambaye sasa anachezea klabu ya Saudi Pro League ya Al Nassr, aliichezea Ureno dakika 90.
Juhudi za Hojlund katika dakika ya 78 zilimaanisha alifunga katika mechi mfululizo kwa klabu na nchi baada ya kumaliza ukame wa mabao 21 dhidi ya Leicester kwenye Ligi ya Premia wikendi iliyopita.
Ushindi ulistahili kwa Wadenmark, na mkufunzi mpya Brian Riemer, na wataelekea Lisbon kwa mechi ya mkondo wa pili Jumapili wakiwa wamejiamini.
Awali Christian Eriksen alipata mkwaju wa penalti wa kipindi cha kwanza uliookolewa na Diogo Costa, ambaye aliruka upande wake wa kulia na kuuwahi mpira huo ukielekea kona.
Download/Pakua/Install App ya Abedijr kupitia google crome Bofya Hapa
app hii aipatikani google playstore ka sasa hupatikana kwenye wavuti yetu hii



No comments