Subscribe Us

Breaking News

YANGA HESABU KWA TABORA UNITED


MILOUD Hamdi, Kocha Mkuu wa Yanga amesema watapambana kufanya kazi kubwa mbele ya Tabora United ili wapate pointi tatu muhimu katika mchezo ujao unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa ndani ya dakika 90.

Machi 2025 Yanga ilifunga kwa kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Songea United mchezo wa CRDB Federation Cup ilikuwa ni Machi 29 ambapo mabao yalifungwa na Duke Abuya dakika ya 22 na Jonathan Ikanga Lombo dakika ya 54.

Kwenye mchezo huo uliochezwa Uwanja wa KMC, Complex nyota wa Yanga Pacome Zouzoua alichaguliwa kuwa mchezaji bora na kupewa zawadi ya laki tano na mdhamini benki ya CRDB.

Miloud amesema wachezaji wanajituma kwenye kutafuta ushindi jambo ambalo linawapa nguvu kushinda na kila mchezo wanautazama kwa umuhimu ndani ya uwanja.

“Kila mchezo ambao tunacheza kwetu tunauchukulia kwa umuhimu ambacho tunahitaji ni kupata pointi tatu, mashabiki wazidi kuwa nasi kwani tunatambua mchezo ujao utakuwa ni wa ligi na ushindani ni mkubwa.”

Mchezo ujao kwa Yanga kwenye ligi ni dhidi ya Tabora United unatarajiwa kuchezwa Aprili 2 2025 kwa vinara hao wenye pointi 58 kushuka uwanjani.



Download/Pakua/Install App ya Abedijr kupitia google crome Bofya Hapa

                               app hii aipatikani google playstore ka sasa hupatikana kwenye wavuti yetu hii 

No comments