Home - ABEDI JR

  • Home
  • Features
  • _Multi DropDown
  • __DropDown 1
  • __DropDown 2
  • __DropDown 3
  • _ShortCodes
  • _SiteMap
  • _Error Page
  • Documentation
  • _Web
  • _Video
  • Download This Template
  • Custom Menu 01
  • Custom Menu 02
  • Normal Link 01
  • Normal Link 02
  • Disclaimer
  • Terms
  • Policy
Home - ABEDI JR
  • Home
  • About
  • Contact
HomeMichezoSIMBA SC KWENYE HESABU NYINGINE KUBWA

SIMBA SC KWENYE HESABU NYINGINE KUBWA

Vijana Brand 6/30/2025

FADLU Davids, Kocha Mkuu wa Simba SC amesema kuwa kwa msimu wa 2024/25 wamejitahidi kupambana na kufikia malengo licha ya kushindwa kutwaa ubingwa watafanya maboresho kwa msimu ujao.

Kuna asilimia chache kwa Fadlu kubaki ndani ya kikosi cha Simba SC msimu wa 2025/26. Taarifa zinaeleza kuwa uongozi wa Simba SC unafanya mazungumzo na kocha huyo ili aendelee kubaki ndani ya kikosi hicho.

Rekodi zinaonyesha kuwa baada ya kuongoza mechi 30 ni ushindi kwenye mechi 25, sare 3 na imepoteza mechi 2. Mechi hizo mbili ni Kariakoo Dabi dhidi ya Yanga SC.

Kwenye mzunguko wa kwanza ilikuwa Simba SC 0-1 Yanga SC na mzunguko wa pili, Yanga SC 2-0 Simba SC. Ni mabao matatu Simba SC imefungwa huku Yanga SC ikiwa haijafungwa.

“Tulikuwa na msimu wenye ushindani mkubwa na kwa kiasi chake tumefikiwa malengo licha ya kutokufurahia yale ambayo yametokea. Kushindana na Yanga SC tukiwa na wachezaji ambao bado nwanazidi kuimarika inatupa nguvu kujipanga zaidi kwa wakati ujao.

“Tutazungumza na uongozi kuona namna yakufanya maboresho katika kikosi. Ninawapongeza mashabiki kutokana na kuwa nasi kwenye kila hatua.”

Mabingwa wa ligi ni Yanga SC chini ya Kocha Mkuu, Miloud Hamdi. Pointi zao kibindoni ni 82 huku safu ya ushambuliaji ikifunga mabao 83. Simba SC nafasi ya pili pointi 78 na safu ya ushambuliaji imefunga mabao 69.

Tags
Michezo
  • Facebook
  • Twitter
  • Newer

  • Older

Vijana Brand

Posted by Vijana Brand

You may like these posts

Post a Comment

0 Comments

Subscribe Us

Social Plugin

Facebook

Tags

Advertisement

Menu Footer Widget

  • Home
  • About
  • Contact
Created By Blogger Theme | Distributed By Gooyaabi Templates

Contact form