Subscribe Us

Breaking News

Shambulio la Urusi lawaua watu 11 katika mji karibu na Donetsk, Ukraine yasema


h

CHANZO CHA PICHA,DONETSK EMERGENCY SERVICE

Takriban watu 11 wameuawa na wengine 30 kujeruhiwa katika shambulizi la Urusi katika mji wa Dobropillya, ulioko mashariki mwa mkoa wa Donetsk nchini Ukraine, mamlaka ya Ukraine imesema.

Majengo manane ya makazi na jengo la utawala yaliharibiwa katika shambulio hilo la Ijumaa, huduma ya dharura ya kikanda ziliripoti. Mji huo uko kaskazini-magharibi mwa jiji la Donetsk linaloshikiliwa na Urusi.

Ripoti hiyo pia ilisema vikosi vya Urusi vilianzisha shambulio la pili dhidi ya wahudumu wa dharura wakati walipokuwa wakipambana na moto uliowaka kutokana na shambulizi hilo.

Hii inakuja baada ya mapigano makali katika maeneo ya karibu, huku waendesha mashtaka wa Ukraine wakiripoti kuwa watano waliuawa katika mashambulizi ya Urusi Alhamisi usiku.




Download/Pakua/Install App ya Abedijr kupitia google crome Bofya Hapa

                               app hii aipatikani google playstore ka sasa hupatikana kwenye wavuti yetu hii 

No comments